mashindano ya qurani

IQNA

IQNA – Washiriki wa kitengo cha wanawake katika Mashindano ya 48 ya Kitaifa ya Qur’ani Tukufu nchini Iran waliendelea kuonesha umahiri wao siku ya tatu ya mashindano hayo, wakishindania nafasi za juu.
Habari ID: 3481412    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/25

IQNA – Waziri wa Mambo ya Waqf wa Misri ametoa pongezi zake kwa kuenziwa hivi karibuni kwa Qari maarufu Sheikh Abdul Fattah Taruti wakati wa mashindano ya kimataifa ya Qur’ani yaliyofanyika mjini Moscow, Russia
Habari ID: 3481409    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/24

IQNA-Sheikh Mamosta Fayeq Rostami, msomi maarufu wa Ahul Sunna na mwakilishi wa watu wa Kurdistan katika Baraza la wanazuoni Wataalamu wanaomchagua Kiongozi Muadhamu wa Iran amesisitiza kuwa Qurani Tukufu si tu kitabu cha ibada, bali ni waraka kamili unaoelekeza maisha ya binadamu katika nyanja za uchumi, utamaduni na siasa
Habari ID: 3481387    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/20

IQNA-Awamu ya mwisho ya Mashindano ya Kitaifa ya Qur’ani Tukufu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ya 48 imezinduliwa rasmi katika hafla iliyofanyika asubuhi ya Jumamosi katika mji wa Sanandaj, mkoa wa Kurdistan.
Habari ID: 3481386    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/19

IQNA-Hafla ya kuvienzi vyuo vikuu vilivyofanya vyema pamoja na kamati ya majaji walioshiriki katika Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani ya vyuo vikuu, yaliyopewa jina la "Al-Nur", imefanyika katika Chuo Kikuu cha Al-Ameed nchini Iraq.
Habari ID: 3481380    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/18

IQNA – Toleo la pili la Mashindano ya Kimataifa ya Usomaji na Kuhifadhi Qur’ani Tukufu nchini Kazakhstan limehitimishwa kwa hafla rasmi iliyofanyika mjini Astana.
Habari ID: 3481378    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/18

IQNA – Chuo Kikuu cha Al-Ameed kimeandaa Mashindano ya Kimataifa ya Qur'an yanayojulikana kama “Qur'an Al-Nur”, yakihusisha wanafunzi kutoka zaidi ya vyuo vikuu 60 vya ndani na nje ya Iraq.
Habari ID: 3481375    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/17

IQNA – Hatua ya mwisho ya Mashindano ya 26 ya Qur'ani Tukufu ya Sheikha Hind bint Maktoum imeanza rasmi Dubai, ikiwakutanisha wanaume na wanawake wanaohifadhi Qur’ani kutoka kote katika Muungano wa Falme za Kiarabu.
Habari ID: 3481372    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/15

IQNA-Idara Kuu ya Mambo ya Kiislamu, Awqaf na Zakat ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) imetangaza kuanza kwa usajili wa toleo la pili la Emirates International Quran Award.
Habari ID: 3481367    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/14

IQNA – Mashindano ya kuhifadhi Qur'ani Tukufu yatafanyika wakati wa toleo la pili la Maonyesho ya Kimataifa ya Vitabu ya Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Libya, yatakayofanyika mjini Tripoli mwishoni mwa mwezi huu.
Habari ID: 3481363    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/13

IQNA – Mashindano ya 48 ya Kitaifa ya Qur'ani Tukufu ya Iran, yakihusisha washiriki 330 kutoka maeneo mbalimbali ya nchi, yatafanyika mwaka huu katika mji wa Sanandaj ulioko magharibi mwa Iran, chini ya kauli mbiu: “Qur'ani, Kitabu cha Umoja.”
Habari ID: 3481362    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/13

IQNA – Mtaalamu mkongwe wa Qur'an, Abbas Salimi, amesema kuwa mashindano ya Qur'an yana mchango mkubwa katika kuimarisha jamii na kuzuia Qur'an Tukufu kusahaulika au kuwekwa pembeni.
Habari ID: 3481352    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/11

IQNA – Qari maarufu wa Iraq na mtangazaji wa televisheni Sayyid Hassanayn al-Hulw ameisifu mashindano mapya ya Qur’an ya Iran yaliyopewa jina la “Zayin al-Aswat”, akiyataja kuwa jukwaa la mabadiliko linalofichua vipaji vya kipekee vya vijana na kuimarisha misingi ya elimu ya Qur’an.
Habari ID: 3481340    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/08

IQNA – Mashindano ya Qur'an kama ‘Zayin al-Aswat’ huwapa vijana msukumo wa kiroho na hutoa kipimo sahihi cha maendeleo yao katika usomaji wa Qur'an, amesema Qari maarufu kutoka Iran, Ahmad Abolqassemi.
Habari ID: 3481337    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/07

IQNA – Profesa Abdul Karim Saleh, Mkuu wa Kamati ya Mapitio ya Qur’ani ya Al-Azhar, ametangazwa na kupewa heshima kama “Mtu wa Mwaka wa Qur’ani” katika Tuzo ya 13 ya Kimataifa ya Qur’ani ya Libya.
Habari ID: 3481331    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/05

IQNA – Qari kijana kutoka Iran aliyeshiriki katika toleo la kwanza la mashindano ya Qur’ani ya ‘Zayin al-Aswat’(mapambo ya sauti) amesifu ubora wa mashindano hayo na kuyataja kuwa fursa muhimu ya kutambulisha wasomaji wa Qur’ani wasiojulikana sana nchini.
Habari ID: 3481323    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/03

IQNA – Hafla ya kufunga mashindano ya kwanza ya kitaifa ya Qur’ani yenye jina “Zayen al-Aswat” (mapambo ya sauti) ilifanyika siku ya Alhamisi mjini Qom, ambapo washiriki bora walienziwa na kutunukiwa zawadi.
Habari ID: 3481322    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/03

IQNA – Mkurugenzi mtendaji wa toleo la kwanza la mashindano ya Qur'ani ya kitaifa ya ‘Zayin al-Aswat’ (mapambo ya sauti) amesema kuwa katika mashindano mengi ya Qur'an, kila kitu huisha kwa sherehe ya kufunga na kuwatuza washindi na sasa sekretarieti ya tukio hili la Qur'an inalenga kuandamana na washiriki kupitia mawasiliano endelevu na yenye tija ili kuwafikisha katika viwango vya kitaalamu na vya kimataifa.
Habari ID: 3481314    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/01

IQNA – Ahmad Abolqassemi, Qari mashuhuri kutoka Iran, amesisitiza uwezo wa kipekee wa nchi hiyo katika uwanja wa usomaji wa Qur’ani Tukufu, akipendekeza kuandaliwa mashindano mapya ya kipekee ya “fainali ya mabingwa” kwa washindi wa mashindano ya kimataifa ya Qur’ani, yatakayofanyika nchini Iran.
Habari ID: 3481300    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/29

IQNA – Libya imetangaza washindi wa Tuzo ya 13 ya Kimataifa ya Qur’ani Tukufu, iliyofikia tamati mjini Benghazi kwa ushiriki wa zaidi ya mataifa 70.
Habari ID: 3481299    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/29